ADAMSON & EVACENCIA!
Nilifumbua macho nikaanza kuangaza huku na huko, wala
haikuwa na aja ya kupata maelezo ilikua ni mazingira ya hospitali, mandhari
ilionyesha tu hivyo, nikajiuliza nimefikaje hapa na ni ugonjwa gani
umesababisha nimefika hapa, nilianza kujiuliza bila kupata majibu, sikukumbuka
kama kabla nilishikwa na ugonjwa wowote, wakati huo dribu niliyokua
nimetundikiwa ilikua imebaki kama robo chupa iweze kuisha, ghafla niliona
mlango wa chumba nilichokua ukifunguliwa akaingia nesi, alikuwa akitabasamu
akaja karibu kabisa na kitanda nilichokua nimelala akaniinamia kasha kwa sauti
ya upole akaniambia ‘’pole dada unajiskiaje kwasasa?’’ nikamjibu ‘’ahsante
nesi’’ akaniambia anaitwa nesi Annastazia, akaniambia nipo ST.Mary Hospital,
uliletwa hapa ukiwa umepoteza fahamu, unaweza kukumbuka chochote kilicho kupata
mpaka hali ikawa hivi? Waliokuleta walisema ulikua H & G Hotel wakakuona
kama umepatwa na mshtuko na ukapoteza fahamu, ndio wakakukimbiza hapa, baada ya
nesi Anastazia kuyasema hayo nikajikuta nikisema Adamson Adamson Adamson,
nilitamka jina hili kwa kigugumizi na kuweweseka hatimae nikaona giza likiingia
machoni hatimae nikazimika! Nilipozinduka kwa mara nyingine tena walas
sikuhitaji maelezo yoyote yakunikumbusha nini kilichotoke kabla ya kufikishwa
hapa, nilianza kukumbuka kilichotokea mchana wa siku hiyo, nilikua H & G
Hotel, hotel ambayo tulipendelea sana kukutana na mpenzi wangu Adamson, na
kukumbuka ilikua siku ya jumamosi nilifika hotelini majira ya saa nane na nusu
kwa miadi ya kukutana na mpenzi wangu huyo ambaye alikua bado yupo kazini,
Hoteli ilikua na ghorofa nne na ghorofa ya nne ndio kulikua na huduma ya
mgahawa, nilifika kwenye meza moja iliyokua karibu kabisa na dirisha ambapo
ningeweza kuona mandhari kubwa ya mji pia barabara na sijui ni kwanini nilihisi
mpenzi wangu angetokea upande huo. Ingawa nilikua sijaonana nae kwa siku moja
tu nilihisi kummisi sana, hakika tulipendana ukizingatia majina yenyewe ndio
hivyo tena yeye Adamson na mimi Evacencia, au Eva.
***
Nikiwa nipo kwenye lindi la mawazo kwa mbali nikamuona
mahabuba wangu akitokeza upande wapili wa barabara alikua akija kwa mikogo,
kweli kutokea kwenye mwendo wake niligundua hata yeye alikua amenimisi, alikua
akitembea kwa haraka lakini kwa mikogo huku akiwa ameweka headphone, sijui hata
alikua akisikiliza mziki gani, mwanaume alinimaliza huyuu!! Hata sijui
aliniloga na nini?, sio siri nampenda sana na naamini hata yeye ananipenda
sana, ghafla alikua anavuka barabara nikiwa nimetingwa kumuangalia likatokea
gari lililotoka na kumvamia mpenzi wangu, kwakweli sikumbuki kilichoendelea
kwani nilipatwa na mshtuko mkubwa, nikapatwa na giza machoni baadae nikazimika
kabisa. Nilipokua naendelea kukumbuka hayo nikamuona nesi Anastazia akiingiia
Tabletop Safety Razor - titanium fitness
ReplyDeleteOne of the best selling safety razors of the era is the Silver Dragon. titanium fishing pliers It is constructed with an titanium joes aluminium alloy and can be attached titanium rod in leg to the titanium piercing jewelry top of the titanium dive watch razor